BENKI YA BIASHARA TANZANIA YAPATA FAIDA YA SHILINGI BILIONI 19.7
Benki ya Biashara Tanzania imepata faida kabla ya kodi Shilingi bilioni 19.7 kwa mwaka unaoishia 31 Desemba 2021. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Dkt. Edmund B. Mndolwa, aliwaambia waandishi wa habari wakati wa Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa Benki hiyo kuwa Benki ya Biashara Tanzania imeendelea kuimarika kwa kutengeneza faida kubwa hadi kufikia faida kabla ya kodi ya Shilingi bilioni 19.7.